MAARIFA ZAIDI
Maisha ni Mfumo halisi katika ulimwengu halisi
Katika maisha hakuna kuigiza au mazoezi kila jambo unalolifanya lina matokeo yake
Na matokeo haya wengine tunaweza yaita ni matunda
Na matokeo haya ambayo yanaibuka baada ya jambo ulilolifanya au kuliwaza au kuliongea huweza kuwa chanya au hasi
Mara zote hakuna binadamu ambaye yuko tayari katika maisha yake binafsi akutane na matokeo hasi... siku zoooote hupenda apate chanya tu katika maisha yake...
Lakini kati ya wanadamu weeengi ambao wanataka wao wewe na chanya tu katika maisha yao hasa kwa matendo na maamuzi wafanyayo lakini pia hupenda sana hata ndugu na jamaa na marafiki na majirani walete mchango chanya katika maisha yao
Mithali 31:12
[12]Humtendea mema wala si mabaya,
Siku zote za maisha yake.
Ukisoma huu mstari kuna jamno hapo
Lakini pia katika maisha yetu wanadamu tunawaza mengi na kufanya mengi lakini Mungu hutuwazia mema.
Katika Zaburi ya 23:6
Anazungumzia swala la fadhili za Bwana kumfuata siku zooooote za maisha yake.....
Endapo ukifanya yampendezayo Mungu basi tegemea fadhili na baraka za Bwana kuwa juu yako....
Lakini pia sio kwa Mungu tu hata kwa Jirani yako, ndugu, rafiki, na wengineo wote ukitaka wakuwazie mawazo mema na kukutendea yaliyomema jifunze kutenda mema kila siku kwao na ukiwakosea jifunze kuomba radhi
Jambo usilopenda kutendewa hakikisha humtendei jirani yako....
Kutoka 20:16
[16]Usimshuhudie jirani yako uongo.
Zaburi 101:5
[5]Amsingiziaye jirani yake kwa siri,
Huyo nitamharibu.
Mwenye macho ya kiburi na moyo wa majivuno,
Huyo sitavumilia naye.
Mithali 11:9
[9]Asiyemcha Mungu humpoteza jirani yake kwa kinywa chake;
Bali wenye haki watapona kwa maarifa.
Marko 12:31
[31]Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi.
Warumi 15:2
[2]Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.
Hii ni baadhi tu ya Mistari kwenye Biblia inayoonyesha ni vyema kutenda mema kwa Jirani yako
Na hii itakusaidia kustawi katika maisha yako maana hataacha kukuwazia mema na kukufanya kupata mrejesho chanya toka kwa kwao.....
Mwisho: Hakuna ambaye anapenda kuwa na rafiki au jirani asiyefanana na malengo yake au kuendana na mfumo wake wa maisha. Lakini tambua kila mtu anakusudi katika Maisha yako ya kila siku. Usimdharau yeyote kwa umri, kipato, jinsia, au namna yoyote ile... Biblia inasema Hata wabaya waliumbwa kwa wakati wa ubaya.... Upendo ndio silaha yetu....
Upendo Huvumilia, Hauhesabu mabaya.........
Wakolosai 3:14
[14]Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.
2017--Maarifa Akilini, Speed Unyayoni
THINK AND GLOW RICH Inspirational and Motivational Inc
No comments:
Post a Comment