SAFARI YA COMORO:
Ndugu wana Yanga kama mnavyofahamu timu yetu ipo ktk maandalizi ya mechi za Club Bingwa Africa. Mechi yetu ya kwanza tunaanzia Moroni Comoro tarehe 12/2/2017.
Wale wanaohitaji kwenda kuisupport timu yetu pendwa taratibu za usafiri ni kama ifuatavyo:
1. Ndege ya bei nafuu ni ATCL karibia USD 430 kwenda na kurudi ingawa inaweza kupungua tukienda kama group. Dirisha la nauli kwa mwezi Feb inataraji kufunguliwa leo au kesho tutawajulisha nauli halisi.
2. ATCLl inafanya safari zake huko siku 3 kwa wiki J4, Alhamis na Jumamosi. Hivyo tarehe nzuri ya mashabiki kusafiri ni 11/2/2017 na kurudi 14/2/2017
3. Visa ni 'on arrival' uenda malipo ya visa yasizidi USD 50 au chini ya hapo
4. Kwa waliokusudia kusafiri ni sharti uwe na Passport ya kitabu iwe haita kwisha muda wake kabla ya tarehe 14/2/2017
Pia cheti cha kinga ya homa ya manjano(yellow fever)
5. Wale wote walio tayari mnaombwa kujiorodhesha hapa au club ili iwe rahisi kufanyiwa wepesi wa safari yetu kwa kuhusisha uongozi wa club, tunafanya mawasiliano na Katibu wetu wa Yanga juu ya safari hii.
SHIME WANA YANGA MSIMU WETU NDIO HUU. TUONYESHE MSHIKAMANO WETU TWENDENI KWA WINGI TUWAPIGIE HUKOHUKO KWAO.
DAIMA MBELE
Monday, January 23, 2017
SAFARI YA COMORO:
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment