Friday, January 19, 2018

UKWELI JUU YA MAMBO AMBAYO MWANAMKE ANAYAHITAJI TOKA KWA MWANAUME.

UKWELI JUU YA MAMBO AMBAYO MWANAMKE ANAYAHITAJI.

Bwana Yesu Asifiwe, moja ya mambo yanayoleta shida kwa wakaka wengi ni kushindwa kujua ya kwamba kibiblia kuna vitu vya msingi ambavyo wadada wanavihitaji maana yake ni vya kwao by nature and you cannot separate it from them, it's unique designed.

Suala la kuokoka haliondoa kile ambacho mdada anakihitaji isipokuwa linaboresha lile jambo ambalo shetani aliharibu baada ya anguko, hivyo tunategemea mtu anapookoka atasimama ipasavyo katika kujua mambo ambayo mdada anayahitaji, jambo hili kwa wadada wengi hawaliona nakujikuta wengi mahusiano yao yakiharibika kwa sababu wakaka wengi waliookoka wanahisi kila kitu duniani ni maombi tu

1. Wadada wanahitaji upendo wa dhati, means kupendwa, hii ndiyo raha yao, muda wote shauku yao, waone mtu aliyepotayari kupenda, why wanajiona ya kuwa wapo salama kabisa and protected, jambo ambalo wakaka wengi huhisi wapo kimwili, ninakuhakikishia kama upo kwenye mahusiano na mdada huonyeshi kumpenda kwa dhati, ni vyepesi mdada huyo huyo ukamkuta tayari haupo ndani ya moyo wake kwa sababu anakuona haupo serious kwake.

Mdada katika maisha yake yote hutasikia akilalamika ya kwamba mkaka hamuheshimu isipokuwa utakuta akilalamika yakwamba hapendwi.

Na mkaka case yake kubwa hutakuta akilalamika yakwamba hapendwi isipokuwa utakuta analalamika yakwamba haheshimiwi

Ni vizuri kujua uhitaji wa kila pande, hata kama ni ngumu kumeza jitahid tu kujifunza itakusaidia.

2. Wadada wanahitaji sana mawasiliano na kuzungumzishwa, yaani ni hatari sana, katika uchunguzi wangu wakaka wengi si wazungumzaji, asilimia kubwa si wazungumzaji kabisa, lakini mdada anakifeel vzr akizungumzishwa, mawasiliano, na hii imekuwa ni vita kwa wakaka wako busy na huduma🙈, hawana tyme hata ya kuwasemesha wadada, muda wote ni prayer, Bwana Yesu asifiwe mama, umesoma Yeremia, wakimaliza hapo ndiyo kamaliza, mim nakueleza utaachwa saa tatu kamili asubuhi, maandiko yanasema tukae nao kwa akili, means lakiza ujitahidi kujua nini wanahitaji.

3.Mdada ni ngumu kuweka mambo na kuyatunza moyoni mwake sana ndiyo maana akiyasema anakuwa huru ndani ya moyo wake tofauti na mkaka ambaye yupo tayari kukaa nayo kwa muda mrefu, ni muwazi siku zote na asilimia kubwa ni waaminifu, msinikasirikie wakaka😊

Kwani ukimuita jina zuri utachubuka? upako utaisha? mnatia aibu sana🙈, ndiyo maana mkaka kumwambia umependeza haoni chochote, mwambie mdada uone, ina add value kubwa sanaa..

4. Urafiki, Kiwango kikubwa cha mahusiano mazuri ni urafiki, hiki ni kiwango ambacho mdada anakihitaji sana, mambo yake anayopitia wakwanza kujua awe mkaka anayetegemea kuwa mume wake, hata kama umeoa na kuolewa tayari mnahitaji kumentain urafiki, Isaka na Rebecca walikuwa marafiki kitu ambacho kilipelekea Mfame kujua ya kuwa siyo dada yake baada ya kuwaona wakicheza cheza, unadhani walikuwa wanacheza rede, mdako au kombolela? The highest Relationship is built into friendship 😋

5. Shauku ya kuuliza maswali, wanapenda sana kuuliza uliza maswali mengi, means wanataka kuelewa zaidi, awe na uhakika, jambo linalowakera sana wakaka wengi maana hawataki kuulizwa ulizwa maswali.

Hii ndiyo furaha yao, kuuliza maswali pale jambo linapoonekana kutoeleweka vzr kwao, ila kwa wakaka wengi huwa siyo watu wa kuuliza uliza maswali mengi kama wadada, hivyo tuwaelewe tu ndivyo walivyoumbwa.

Sasa wadada wengi hata kama wanauliza maswali mengi lakini hawajui kwa nini wao asili yao hujikuta wakiuliza maswali mengi kwa wakaka kiasi kwamba wakaka wengi wamewaogopa wadada kwa sababu ya maswali yao.

Kadharika na wakaka nao hawajui kwa nini wanaulizwa  maswali mengi

Jibu ni hili, Mungu alimpatia Adamu maelekezo ya namna ya kuishi katika bustani ya Edeni, na hayo maelezo Adam akamueleza Eva, hivyo Eda kuuliza maswali ni kutaka kujiridhisha juu ya maelezo aliyopewa Adam na Mungu, kumbuka ukiona mdada anakuuliza maswali mengi ni kwa ajili ya usalama wako ila mpaka awe mdada mwenye hofu ya Mungu vinginevyo atachuma matunda uliyokatazwa na utakula tu

Si vyepesi sana kujua hili suala kwa urahisi, lakini pia ni muhimu sana kufahamu haya mambo itakusaidia mbele ya safari

Wakaka wengi wanakuwa bored wanapoulizwa ulizwa maswali 😅, shida ni nini mpaka unakasirika ukibanwa maswali? ndiyo raha yao ujue

Kuna vitu ukiwa rafiki na mdada hautavikuta kwa Mchungaji wako kanisani, urafiki hauna mipaka maana yake atakuwa huru kukueleza

6. Mdada yeyote anashauku ya kusapotiwa kifedha ndani ya moyo wake, hii inaweza isiwe issue kubwa sana kwa wadada wanaofanya kaz, but Mungu alimuweka Adam kwenye bustan ya Eden ili aitunze na kuwa provider kwa familia yake, yes sikushauri hata kidogo mkaka uoe kama huna pesa.

7. Wanapenda sana mtu wa kujitoa katika mambo ya kifamilia, na muda mrefu atakuuliza mambo ya maendeleo ya kifamilia

8. Mdada anatamani kumfuata kiongozi wa familia, mara nyingi hata kama anajua jambo hutamani kujua leader au head of the family anasemaje, sasa mahead of the family wengi hawajitambui hata kidogo wanahisi ubabe ni dawa.

No comments:

Post a Comment