JE, NIINGIE KWENYE MAISHA YA NDOA NA NANI?
Wengi limekuwa jambo gumu sana kutaka kujua aingie kwenye maisha ya mahusiano na ndoa bdae na mtu gani, unisikilize itakusaidia.
1. Hakikisha mtu huyo anamcha BWANA.
Wewe siyo Yesu hadi uokoe, si swala la kuingia na mtu asiyemcha BWANA ukidhani uko salama, maandiko yanasema tusifungiwe nira na mtu asiye amini.
Kuamini nini, kuamini imani ya Kristo Yesu
Neema ya wokovu bado ipo, utashangaa utakapoamua kukubali kuiingia kwenye maisha na mtu asiyeamini imani yako ghafla ameshakuweka ndani anakugeukia, anakwambia kuanzia leo hakuna kwenda kanisani, anakuchekea leo, kesho atakugeuka, moyo wa mwanadamu kama haumjui Mungu ni hatari sana...
Tukumbushane kidogo hapa wapendwa "Kilichomfanya Yusufu amkimbie yule mama mke wa potifa bila kufanya nae dhambi, ilikuwa ni neema ya kumjua Mungu iliyokuwepo juu ya Yusufu", Sasa fikiria ndiyo imemtokea boyfriend wako ambaye hamjui Mungu, kitu gani kitatokea..? (Jitafakari moyoni mweyewee hata usichekee)
Weit my friend God's Fearful relationship itakusaidia kukutunza hata kama mwili utainuka, utastahimili usimtende Mungu dhambi kwa sababu tu ya neema ya kuwa na hofu ya Mungu baina yako na mtu uliyepo kwenye mahusiano, ila kama mmoja hofu ya Mungu haipo, uwe na uhakika hamtaweza kustahimili, trust me.
Mabinti wengi wanaomjua Mungu waliopo makanisani, asilimia kubwa hawako tayari kuolewa na vijana wa kanisa, why,.
Vijana wa kanisani wanaonekana washamba sana, watu wa mabwanga, asante Yesu nilizungumza sababu zinazopelekea wakaka kuachika sana, likiwemo hilo.
Suluhisho.
Mueleze kwa hekima, vaa shati linalokutosha vizuri, vaa suluari zinazokuenea vzr
Akikataa, tulia kwanza, rudi tena, maana ni wabishi kubadili kwa haraka haraka, muombe Mungu akusaidie hadi aelewe.
Nia yangu ni hii, usimuache mkaka kisa anavaa mabwanga, ndiyo maana upo umsaidie awe smart, ili uanze kumtambulisha bila aibu kwa marafiki zako.
2. Mwenye kujua nini anapaswa kufanya kwa mwenzake kutimiza kusudi la yeye kuwa na mwenzake.
3. Aliye tayari kujifunza, kuongozwa na mwanaume huyo, kama haupo tayari kujifunza kwake na kuongozwa naye kama kiongozi wa familia, usikubali akuoe, muache atafute mwingine.
Usikubali kama haupo tayari kuwajibika kwake,
Usikubali kama unaona anapwaya kwenye vigezo vyako, yaani siyo shauku ya moyo wako, usikubali kuwa naye, muache atafute mwingine.
4. Hakikisha amani ya moyo wako kutoka ndani kabisa imekubali kwenda na mtu huyo, yaani mkaka huyo, usiingie nae kisa ana kibanda cha chipsi mayai, usikubali kisa ana kioski, usikubali kisa ana salon ya wadada, usikubali kisa ana gari, usikubali kisa ana nyumba, upendo haujengwi kwa vitu, uwe na uhakika ndani yako uhalisia unakataa, upendo unakuja automatic, love without any reason will sustain your relationship.