Monday, March 27, 2017

MLO KAMILI HASA KWA MAMA MJAMZITO ILA SOMA HII KWANI HATA WEWE ITAKUSAHIDIA..

MLO BORA KWA MAMA MJAMZITO.

Kwa ajili ya afya ya mama na mtoto ni muhimu sana mwanamke apate chakula bora. Ukosekanaji wa chakula bora kunaweza kukasababisha mtoto kuzaliwa kabla ya mda wake au na uzito mdogo ambao unaweza ukachangia katika kuzuia ukuaji wa ubongo na mwili kwa ujumla.

Na endapo mama mjamzito atakosa mlo bora uliombatana na protini anaweza akapata anaemia, infection, matatizo katika placenta, matatizo katika labor, c-section(kuzaa kwa upasuaji wakati wa kujifungua), kutokupona kwa haraka, matatizo katika kunyonyesha, toxemia na pre-eclempisa(haya ni magonjwa yanayosababishwa na maini kutoweza kufanya kazi yake vizuri

Hivyo ili kujenga afya ya mama na mtoto imeshauriwa ya kwamba mama mjamzito anatakiwa apate 100 grams za protein kwa siku.

Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ili kuweza kupata afya bora:

1.Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa:
Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi,siagi, ice cream. Maziwa ni muhimu kwa protein, calcium, vitamins na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa, misuli na nerves. Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mapigo ya moyo.

Mayai:
Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protein, vitamins minerals na vitamin A ambayo itasaidia kuzuia infections.

Vyakula vyenye Protein
Serving mbili ya samaki, maini , kuku, nyama ya ngombe, mbuzi, kondoo au nguruwe, maharagwe au jibini. Kusaidia ujengaji mifupa, meno, misuli, ubongo na mwili kwa ujumla. Ukosekanaji wa protein ya kutosha kutasababisha kuchoka, uvimbe na kutojisikia kula au appetite ndogo.

Mboga za majani.
Spinach, cabbage, collard greends, mchicha, matembele. Mboga hizi ziwe fresh na zile zenye rangi ya kijani iliyokolea(hizi ndio zenye virutubisho vya kutosha).  Mboga hizi zitakupa Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kuabsorb protein ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata anemia.

Vyakula vyenye vitamin C.
Kipande kimoja au viwili vya machungwa au juisi ya ndimu, machungwa, nyanya. Vitamin C itasaidia uterus kuwa na nguvu ya kutosha ili kufanya kazi vizuri wakati wa labor, pia itasaidia kulinda mwili na infection na kusaidia kuabsorb iron kwenye mwili.

Maji ya kunywa.
Kunywa maji mengi ya kutosha. Maji huchangia kwa asilimia 75 ya uzito wa mtoto wako atakapozaliwa. Usipopata maji ya kutosha utaishiwa na nguvu kwa asilimia 20 na kupata matatizo ya dehydration na kichwa kuuma.

Tumia chumvi kiasi.
Chumvi  kusaidia kuzunguka kwa damu kutoka mwilini kwenda kwenye placenta. Kutopata chumvi ya kutosha kunaweza kusababisha miguu kuuma na uchovu.

Kwenye sehemu ya pili tutaongelea virutubisho kadhaa na umuhimu wake kwa mama mjamzito na mtoto. Ila kumbuka utumiaji wa chumvi kwa wingi una madhara kiafya.

MLO KAMILI HASA KWA MAMA MJAMZITO ILA SOMA HII KWANI HATA WEWE ITAKUSAHIDIA..

MLO BORA KWA MAMA MJAMZITO.

Kwa ajili ya afya ya mama na mtoto ni muhimu sana mwanamke apate chakula bora. Ukosekanaji wa chakula bora kunaweza kukasababisha mtoto kuzaliwa kabla ya mda wake au na uzito mdogo ambao unaweza ukachangia katika kuzuia ukuaji wa ubongo na mwili kwa ujumla.

Na endapo mama mjamzito atakosa mlo bora uliombatana na protini anaweza akapata anaemia, infection, matatizo katika placenta, matatizo katika labor, c-section(kuzaa kwa upasuaji wakati wa kujifungua), kutokupona kwa haraka, matatizo katika kunyonyesha, toxemia na pre-eclempisa(haya ni magonjwa yanayosababishwa na maini kutoweza kufanya kazi yake vizuri

Hivyo ili kujenga afya ya mama na mtoto imeshauriwa ya kwamba mama mjamzito anatakiwa apate 100 grams za protein kwa siku.

Ifuatayo ni mlo kamili anaotakiwa apate mama mjamzito kila siku ya ili kuweza kupata afya bora:

1.Maziwa na vyakula vya jamii ya maziwa:
Glasi nne au zaidi ya maziwa ya aina yoyote pamoja na/au vyakula vyenye jamii ya maziwa kama jibini, mtindi,siagi, ice cream. Maziwa ni muhimu kwa protein, calcium, vitamins na virutubisho vingi. Vitasaidia ukuaji wa mifupa, misuli na nerves. Ni muhimu kwa damu yenye afya, kusaidia usingizi na kusawazisha mapigo ya moyo.

Mayai:
Mayai mawili kwa siku husaidia kuupa mwili protein, vitamins minerals na vitamin A ambayo itasaidia kuzuia infections.

Vyakula vyenye Protein
Serving mbili ya samaki, maini , kuku, nyama ya ngombe, mbuzi, kondoo au nguruwe, maharagwe au jibini. Kusaidia ujengaji mifupa, meno, misuli, ubongo na mwili kwa ujumla. Ukosekanaji wa protein ya kutosha kutasababisha kuchoka, uvimbe na kutojisikia kula au appetite ndogo.

Mboga za majani.
Spinach, cabbage, collard greends, mchicha, matembele. Mboga hizi ziwe fresh na zile zenye rangi ya kijani iliyokolea(hizi ndio zenye virutubisho vya kutosha).  Mboga hizi zitakupa Vitamin A na B, pia virutubisho vitakavyosaidia mwili kuabsorb protein ya kutosha, ukuaji wa mwili, na utengenezaji wa damu. Kutopata mboga za kutosha kunaweza sababisha mama kupata anemia.

Vyakula vyenye vitamin C.
Kipande kimoja au viwili vya machungwa au juisi ya ndimu, machungwa, nyanya. Vitamin C itasaidia uterus kuwa na nguvu ya kutosha ili kufanya kazi vizuri wakati wa labor, pia itasaidia kulinda mwili na infection na kusaidia kuabsorb iron kwenye mwili.

Maji ya kunywa.
Kunywa maji mengi ya kutosha. Maji huchangia kwa asilimia 75 ya uzito wa mtoto wako atakapozaliwa. Usipopata maji ya kutosha utaishiwa na nguvu kwa asilimia 20 na kupata matatizo ya dehydration na kichwa kuuma.

Tumia chumvi kiasi.
Chumvi  kusaidia kuzunguka kwa damu kutoka mwilini kwenda kwenye placenta. Kutopata chumvi ya kutosha kunaweza kusababisha miguu kuuma na uchovu.

Kwenye sehemu ya pili tutaongelea virutubisho kadhaa na umuhimu wake kwa mama mjamzito na mtoto. Ila kumbuka utumiaji wa chumvi kwa wingi una madhara kiafya.

Friday, March 17, 2017

UKIENDELEA NA TABIA HIZI MAFANIKIO KWAKO YATAKUWA NI NDOTO

UKIENDELEA NA TABIA HIZI MAFANIKIO KWAKO YATAKUWA NI NDOTO.

Hasira za mafanikio zinatofautiana baina ya mtu mmoja na mwingine. Kama kweli unahitaji mafanikio ya kweli ni lazima uwe na hasira ya njaa kama aliyonayo simba. Miongoni mwetu ni watu wachache sana wanatambua hasira hii ya mafanikio, wengi wetu huchukulia mafanikio kwa sura ya kawaida sana na mwisho wa siku tunaishia kuwa maskini.

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana, nasema hivi ni kiwa na maana ya kwamba binadamu anapenda sana maisha ya kufanyiwa kila kitu, kwa mfano mtu anapenda umpikie chai, umuwekee kwenye chupa, umuwekee chai kwenye kikombe na umgorogee na sukari katika chai na ukishamfanyia yote hayo subiri anywe hiyo chai uone atakavoanza kulaamu utamskia anasema sukari imezidi au sukari hajikolea na lawama zingine nyingi, kitu cha kujiuliza je, mtu huyo alishindwa kuweka sukari mwenyewe kwenye chai yake ili jambo lolote likitokea akose wa kumlamu.

Mtu huyo huyo ukimuuliza unafanya biashara gani? Utamsikia anasema sifanyi biashara yeyote ile mi nipo tu, ukimuuliza kwanini haufanyi biashara yeyote tatizo nini? Atamsikia anakujibu tatizo mtaji huku akiamini kuwa mataji pekee katika biashara ni fedha. Ndugu msomaji wa makala hii hata uwe na fedha kiasi gani kama huna wazo kwa ajili ya matumizi ya fedha, hata ukipewa milioni mia moja leo hizo pesa zitaisha utajikuta mwisho wa siku huna hata mia mbovu. Watu wengi tunatazama mitaji kama fedha peke yake ukitazama katika msingi huo utazidi kulamu mpaka mwisho huku maisha yakiendelea kuwa magaumu.

Ngoja nikuibie siri mtaji unaweza ukaupata kwa kutumia ujuzi pamoja nguvu ulizonazo ili kutengeneza bidhaa au huduma zitazokufanya upate fedha. Kwa mfano Wewe mwenye elimu juu tekinologia ya habari na mawasiliano unaweza ukabili ujuzi wako kuwa bidhaa kwa kuwa fundi wa computer na kutengeza progamu mbalimbali. Swali la kujiuliza unaweza vipi kubadili ujuzi ulio nao kuwa bidhaa au huduma hapo ndipo wengi tunapofeli kwa sababu ni wavivu wa kufikiri.

Naendelea kumchambua binadamu ili uone ni jinsi gani tulivyokuwa na tabia za lawama. Binadamu huyo huyo utamkuta anaishi mazingira machafu ambayo yatasababisha muda wowote magonjwa ya mlipuko kutokea, ukimfuta binadamu huyo na kumuuliza unafikiri ni kwanini mazingira haya ni machafu, utamsikia jibu atakalokupa atakwambia tatizo ni serikali, binadamu huyohuyo utamkuta hana ajira ila ukimuuliza kwanini hauna ajira? Atakujibu tatizo ni serikali.

Kuna msanii mmoja wa hapa nchini aliwahi kuimba kwenye wimbo huku akiuliza serikali ni nini? Maana imekukuwa ikutupiwa lawama kwa kila kitu. Ndugu msomaji wa makala haya nakusihi na kukushauri pia kwa kile ambacho unaweza kukifanya usisubiri serikali ndio ukifanyie, kama unauwezo wa kufanya usafi katika eneo lako fanya usisubiri kuambiwa, maana tabia za bianadamu kwa asilimia kubwa wanasubiri kuambiwa fanya hiki fanya kile . UKisubiri kuambiwa maisha ya mafanikio kwa upande wako yatakuja kwa asilimia chache sana.

Kitu cha msingi ya kuzingatia ni kwamba tuache lawama sizisokuwa na msingi wowote, kwani lawama ulizonazo leo hata yule unayemlalamikia hakusikii na unazidi kuwa maskini tu. Jambo la msingi fanya kila kitu kwa moyo mmoja bila kusubiri mtu fulani akwambie ufanye. Daima tukumbuke usemi huu “ kila uonapo nyundo usifikiri kila tatizo ni msumari’’

Mafanikio ya kweli huja kwa mtu kujitambua yeye ni nani? Na ni kwanini upo hapo ulipo. Kuna usemi mmoja hivi wa kiswahili unasema kila binadamu ni mchungaji ,kama ndivo hivyo basi kama mimi leo nikiulizwa nimechunga nini, jibu langu litakuwa lipo wazi ya kwamba natumia muda mwingi kuwafunza watu ili kujua mbinu za kufanikiwa, je wewe mwenzangu unasoma makala hii endapo utaulizwa swali kama hilo utajibu nini? Tafakari kisha uone una thamani gani mbele ya watu wengine?.

Wednesday, March 15, 2017

WEWE NI MTOTO WA NGAPI KUZALIWA?

WEWE NI MTOTO WA NGAPI KUZALIWA? 👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇👇 FAHAMU NGUVU ZAKO ZA KUZALIWA KWA UFUNUO WA ROHO MTAKATIFU

Kumb 33:1-9, Mwanzo 49:3-7, 1Kor 2:10
Kila mwanadamu aliyeumbwa na Mungu Aliye Hai, ameumbwa na nguvu maalumu kutoka mbinguni, ambayo ni mtaji wake maalumu; kiroho, kijamii na kiuchumi.
Mwanzo 49:3
Reubeni u mzaliwa wangu wa kwanza,nguvu zangu na malimbuko ya uwezo wangu. Umewapita wengine kwa ukuu na nguvu.

1. MZALIWA WA KWANZA KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Amebeba nguvu nyingi za familia.
ii. Amebeba Baraka za aina mbalimbali za wadogo zake.
iii. Amebeba nguvu ya upendo ndani ya familia.
iv. Mzaliwa wa kwanza ni lango, Zab 24:7-9, ambapo Baraka zote za familia kutoka mbinguni zinapitia kwake na kuwafikia wadogo zake wote.
v. Amebeba ustawi wa familia kiroho na kimwili.

2. MTOTO WA PILI KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Ni m’beba neno la uzima.
ii. Kipawa cha ualimu kinakaa vizuri sana ndani yake.
iii. Amepewa neno la uzima la kusaidia kanisa familia na nchi.

3. MTOTO WA TATU KATIKA FAMILIA YOYOTE:
i. Ni mtawala katika ulimwengu wa roho  na wa mwili.
ii. Ni mtunga sheria popote atakapokuwa anaishi, anasoma au anafanya kazi.
iii. Amepewa mamlaka ya kusimamia jamii, kuiongoza na kuitawala.
iv. Anafaa kuwa mwanasheria au kiongozi popote aendapo.

4. MTOTO WA NNE KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Amepewa neema ya kumiliki utajiri wa nchi.
ii. Kama akijitambua na kusimama katika zamu yake, ajue amepewa neema na nguvu ya kuutawala uchumi vizuri sana.
iii. Amepewa nguvu ya kumiliki utajiri wa mbingu na dunia.

5. MTOTO WA TANO KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Amepewa neema ya kushinda changamoto.
ii. Amepewa stamina ya kushindana na majaribu kwa asili.
iii. Amepewa neema ya kutumika na upako wa juu sana, kama akiokoka na kujitambua, na kusimama katika zamu yake.

6. MTOTO WA SITA KATIKA FAMILIA YOYOTE
Ni mtu wa ujuzi, na talanta.  Na Amepewa nguvu ya ubunifu wa pekee.

7. MTOTO WA SABA KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Amebeba uheri wa Mungu Mtakatifu.
ii. Yeye ni jubilee, yaani maachilio.
iii. Usithubutu kushindana naye maana hautafanikiwa.
iv. Ukimshitaki hauwezi kufanikiwa.
v. Anafaa kuwa mzee wa kanisa.
vi. Anafaa kuwa hakimu kama ataamua kuichukua taaluma hii.
vii. Ukipata kesi yoyote na akakusindikiza ni lazima utashinda, maana utu wake wa ndani ameumbiwa neema hii.

8. MTOTO WA NANE KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Amebeba nguvu ya utumishi.
ii. Amepewa neema ya kusaidia wengi kiuchumi, kiroho na kijamii, kama akijitambua na kusimama katika zamu yake.
iii. Akiokakoka na kuwa mtumishi kanisa lolote, atalisaidia sana kustawi, kwa kuwa ni mtu wa kutegemewa sana.
iv. Amepewa neema ya kuwa nguzo.
v. Ukimtambua katika kanisa lako na kumthamini, na kumtumia vizuri, utafanikiwa sana.

9. MTOTO WA TISA KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Ni m’beba karama.
ii. Akipokea kipawa anakitunza sana kwa muda mrefu.
iii. Amepewa nguvu ya umoja.
iv. Ni mtu anaweza kuinganisha jamii, nchi au familia na kuleta mshikamano.
v. Anafaa kuwa mwanasiasa endapo akijitambua na kusimama katika nafasi yake aliyokirimiwa na mungu.

10.  MTOTO WA KUMI KATIKA FAMILIA YOYOTE
i. Yeye ni msamaha.
ii. Amekirimiwa nguvu ya msamaha.
iii. Amepewa uwezo wa kusuluhisha migogoro kwa ufanisi wa hali ya juu sana.
iv. Anafaa kuwa mzee wa kanisa.

11.   MTOTO WA KUMI NA MOJA KATIKA FAMILIA YOYOTE
Ni faraja kwa familia.
Kuna wakati anapata tatizo la kukataliwa, lakini ni mvumilivu sana.
Mkikaa naye kwa upendo mtabarikiwa sana.
JIULIZE WEWE NI MTOTO WA NGAPI  NAJEE UNAITENDEA VYEMA NAFASI YAKO?

Monday, March 13, 2017

Mvua yaleta mafuriko jijini Dar

https://youtu.be/BHqVGLWoMkI

ACHA KUWA MVIVU MPENDWA SOMA HII

MVIVU

"Mtu yeyote anayekuambia juu ya hatari zilizoko kwenye njia yake kuelekea mafanikio anayoyataka, na anadai ndio sababu ya yeye kuacha kuchukua hatua kuelekea mafanikio, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 22:13).

"Mtu yeyote ALIYEFUNGA NDOA NA GODORO, anafanya kazi ya kugeuza mbavu zake, kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 26:14).

"Mtu anayependa kusukumwa sukumwa, kusimamiwa simamiwa, kuelekezwa elekezwa, kuambiwa ambiwa mambo ambayo alipaswa kujiambia, kujielekeza, kujisukuma, kujisimamia, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 6:6-8).

"Mtu asiyefikiri kuhusu kesho, na kuweka mikakati ya kuikabili hiyo kesho, anasubiri vitu vitokee bila mipango na maandalizi, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 6:6-8).

"Mtu yeyote ambaye mambo yake yako shaghalabaghala, hayana mipangilio, hayana unadhifu, uzuri na ubora, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 24:30-34).

"Mtu yeyote anayeuhurumia mwili wake, na anapenda kujihurumia hurumia, badala ya kuutesa mwili na matakwa yake ya muda mfupi, MTU HUYU NI MVIVU"
(Mithali 20:4).

Mtu yeyote ambaye ukijaribu kumulekeza yampasayo ili afanikiwe, anajitia mjuaji na anakupa sababu nyingi za kwanini haiwezekani, badala ya kwanini aweze, MTU HUYU NI MVIVU
(Mithali 26:16). 

NAIAMURU ROHO CHAFU YA UVIVU IKUTOKE KWA JINA LA YESU.

Saturday, March 11, 2017

MPIRA UMEKWISHA YANGA 1 ZANACO 1 HII NDIYO TATHIMINI KWA TIMU YANGU DAR- YOUNG AFRICAN

MPIRA UMEKWISHA YANGA 1 ZANACO 1
TATHIMINI KWA YANGA SC
George Lwandamina kaianza vyema mechi kwa hesabu za kimbinu na kiufundi. Licha ya kasi na matumizi makubwa ya nguvu aliwaweza kwenye marking na kuwatoa mchezoni kwa kuwatumia Yondani , Zulu , Kamusoko na Ngoma .
Timu imetengeneza nafasi nyingi za kufunga sema utulivu wa forward line ya Yanga kwenye finishing ilikuwa tatizo ukiacha nafasi moja waliyoipata na Msuva kufunga bao dakika ya 39. Ni goli lililotafutwa vizuri kimbinu kazi ikianzia kwa Ngoma akirudi chini kama Play maker na kumpasia Zulu wing ya kulia ambaye kwa utulivu mkubwa anamtengea Msuva ndani ya 18 na yeye akionesha kuwa yupo matured anatengeneza goli zuri.
Nini kimewafanya Yanga kushindwa kulinda goli?
Kwa macho mepesi unaweza mtupia lawama kocha kwa mabadiliko aliyoyafanya kwa kuwatoa Ngoma na Kamusoko na kuwaingia Emanuel Martini na Juma Mahadhi na ndipo Zanaco walipoanza kuja kwa kasi na kutengeneza goli.
Kwanza kabisa ni lazima tukubali jambo moja kabla ya kumtupia lawama kocha . Lazima tuwe na mtazamo sahihi katika kufikiri na kutoa majibu sahihi. Yanga SC kimbinu na kiufundi ina wachezaji wengi ambao ni averaged players . Wachezaji kiwango cha wastani ambao wanakosa basics nyingi kimbinu na kiufundi na hili si kwa Yanga tu ni sehemu kubwa ya nchi yetu kwa sababu hatuna misingi mizuri huko chini.
Ngoma ameingia katika mechi hii akiwa hayupo sawa kwa zaidi ya asilimia 50 lakini 50 zilizobaki ndizo alizotusaidia kuwatuliza wazambia kule mbele na kuanzisha move ya goli. Jiulize asingecheza kabisa ingekuwaje?!. Kocha kamtoa nje baada ya hali yake kuwa tete na kuanza kucheza kwa woga kwa hofu ya kuumia. Hofu yake ilianza kuwapa amani Zanaco na kucheza free. Kocha kamtoa nje na kumwingiza Emanuel ili kuendeleza tempo ya mchezo lakini Martin kapoteza nafasi nne za wazi kwa kukosa utulivu na umakini kimbinu . Lwandamina aingie kucheza ?
Kamusoko majeruhi wa mechi ya watani wa jadi. Leo kaanza kama kiungo mshambuliaji akiwa bado hajapona sawa . Na imelazimika kupangwa baada ya Tambwe kuwa bado majeruhi na Niyonzima kuchelewa mazoezi . Amefanya mazoezi siku mbili tu akikosekana zaidi ya siku sita ! anatoa wapi match fitness?! Apangwe aitwe muhujumu tena ?! au kuvunja morali ya waliotoka jasho juma zima?! Kumpa nafasi Kamusoko GL alicheza vyema kamari lakini kutoneshwa na kuanza kucheza kwa hofu ilimlazimu kocha kumtoa .
Shida moja ya Mahadhi hajatambua kama GL anamwamini na anatamani afanikiwe. Mabadiliko yake kwa Kamusoko yalilenga vitu viwili ambavyo yeye imekuwa tatizo kuvitimiza. Kwanza ku " mantain " mashambulizi na kuhakikisha mpira mbele unakaa na cha pili kuhakikisha muunganiko wake na viungo chini yake unaimarishwa katika " direct play ". Mahadhi kaingia akawa flat & floppy na kuwaruhusu Zanaco kuwa na mipango mizuri toka chini hali iliyofanya kiungo chote cha Yanga kuvamiwa na kumtoa kabisa mchezoni Zulu kwenye mipango ya kushambulia na kujikuta wakijikusanya kati na Yondani bila mwelekeo.
Jicho la GL likaamua kumtoa Zulu na kumleta Kaseke; kwanza awape back up Mahadhi na Yondani pili ajaribu kuisukuma timu mbele . Kidogo hii ilisaidia.
Bado Yanga ina nafasi ya kushinda ugenini endapo hawa majeruhi watakuwa safi na Haruna kucheza . Lakini timu inahitaji " build up " kubwa kiufundi kwa aidha wachezaji kubadilika na kucheza kama matured players wanaoweza kutafuta goli na kulilinda.
Narudia tena tazameni timu yenu , mahesabu wanayotumia waalimu na uwezo wa mchezaji mmoja mmoja kabla ya kumlaumu mwalimu.
Kwanini Zulu hajatumika kama kiungo mkabaji?
Endapo Kamusoko angekuwa vyema kwa asilimia 100 . Yaani mzuri kwenye battling bila hofu ya kujitonesha ? Ni dhahiri kocha angeanza na Zulu chini , Kamusoko juu , Ngoma tisa na kumi Chirwa na pembeni Kaseke lakini Kamusoko na Ngoma wameingia kama kamari hivyo lazima nyuma yao uwape mtu wa back up . Mtu ambaye anaweza kufuta makosa yao kwenye marking pia kuwafungulia njia ili wacheze soka kwenye open space ndio maana Zulu akapangwa juu kama box to box na chini yake Yondani . Ni kama kocha alipandisha ukuta wa marking kwa juu ya Nadir na Bossou kumweka Yondani na amefanya kazi nzuri kabla ya kiungo chao kuvurugwa kwa mabadiliko.
Mtazamo wangu

USIURUHUSU MOYO WAKO ULIPIZE KISASI NA MWL: CHRISTOPHER MWAKASEGE

Usilipize Kisasi! Unasikia? Hata ikiwa umefanyiwa ubaya wa namna gani, Biblia inafundisha na inakusihi usilipize kisasi kwa huyo aliyekufanyia ubaya. Biblia inasema hivi:
" Wapenzi, msijilipizie kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, kisasi ni juu yangu Mimi, Mimi nitalipa, anena Bwana " (Warumi 12:19)
Kuna hasara zinazoweza kukupata ukiamua kulipa kisasi kwa mambo uliyofanyiwa ambayo hayakupendezi. Ikiwa ni masuala ya kikabila, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kidini, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kifamilia, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya kikazi, usilipe kisasi. Ikiwa ni masuala ya uhusiano wako na majirani zako, usilipe kisasi.Ndiyo! Usilipe kisasi! Kwa nini? Kwa sababu " imeandikwa kisasi ni juu yangu Mimi; Mimi nitalipa, anena Bwana ".
Lakini ikiwa utaona ya kuwa Mungu hawezi kukusaidia na ukaamua kujichukulia madaraka ya kujilipiza kisasi hasara zifuatazo hakika zitakupata!
Hasara ya Kwanza "UTASHINDWA!"
Katika jambo lolote lile lililokukasirisha - liwe la kidini, au kikabila, au kifamilia, au kikazi, na kadhalika ukiamua kulipa kisasi utashindwa wewe kwa sababu vita hivyo si vya mwili na wala silaha ambazo Mungu amekupa si za mwili! Tunasema hivi kwa sababu katika  2 Wakorintho 10:3- 5 imeandikwa hivi:" Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi yamwili; maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome, tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo ".
Soma: Tabia 8 Za Watu Wapole - Dr. Chris Mauki.
Tena katika kitabu cha Waefeso 6:12 imeandikwa hivi: " Kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho ".
Uwanja wa mapambano uliyonayo ni " katika ulimwengu wa roho " na mapambano uliyo nayo " si juu ya damu na nyama " - ingawa unaona ya kuwa ni watu na ni binadamu kama wewe wanaokusonga - lakini fahamu hili ya kuwa wanatumiwa tu na ibilisi!
Mbinu mojawapo ya shetani anayotumia akitaka kukuangamiza ni kukufanyia kitu kitakachokukasirisha ili uamue kujibu au kushindana kimwili kwa sababu anajua ukishindana " kimwili " au katika mwili utashindwa hakika, maana vita hivyo si vya mwili wala silaha ambazo Mungu amekupa si za mwili!
Hasara ya Pili "MATATIZO HAYATAKWISHA!"
Kumbuka imeandikwa hivi katika kitabu cha Wagalatia 6:7; " Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote ampandacho mtu. Ndicho atakachovuna ".
Ikiwa umeamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule aliyekufanyia - ubaya hautakwisha, kwa sababu utavuna ulichopanda.Ndiyo maana imeandikwa hivi:" Yeye arudishaye mabaya badala ya mema, mabaya hayataondoka nyumbani mwake " (Mithali 17:13)
Ukiamua kulipiza kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa nyumbani mwako - Biblia inasema " mabaya hayataondoka nyumbani mwako " Hii ndiyo maana matatizo mengi katika ndoa na katika jamii hayaishi - kwa sababu mtu akifanyiwa ubaya naye analipa kisasi.
Ukiamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa nchini mwako ujue hakika mabaya hayataondoka nchini mwako. Hili ndilo lililowapata wenzetu wa nchi za Burundi na Rwanda - kulipizana kisasi - matokeo ni uhasama usiotaka kupotea - pamoja na juhudi zote za kimataifa kutafuta suluhisho.
Ukiamua kulipa kisasi kwa kumfanyia ubaya yule wa kazini kwako - fahamu mabaya hayataondoka kazini kwako. Ikiwa ni shuleni - mabaya hayataondoka hapo shuleni.
Tena hali ya mwisho inakuwa mbaya zaidi,kila wakati kisasi kinapoendelea kupandwa. Kwa sababu ukiwapa watu ubaya - nawe utapewa ubaya kwa; " kipimo cha kujaa na kushidiliwa, na kusukwa sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile upimacho ndicho mtakachopimiwa" (Luka 6:38)
Soma: Jifunze Kusamehe - Mwalimu Christopher Mwakasege
Kumbuka ubaya haushindwi na ubaya mwingine, bali unashindwa na wema kama vile dawa ya chuki si chuki bali upendo! Ndiyo maana Warumi 12:21 inasema; "Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema ".

Tuesday, March 7, 2017

MAFANIKIO YAKO YAMEJIFICHA HAPA

    MAFANIKIO YAKO YAMEJIFICHA HAPA.
                                 👇👇

√Yapo matokeo ambayo katika maisha yako wewe huwezi kuyaona hapo hapo wala mwingine pia hawezi kuyaona kwako. Kwa mfano, unaposoma kitabu huwezi kuona matokea yake leo au kesho moja kwa moja, inachukua muda fulani.

•Kwa hiyo unaona kama yapo matokeo ambayo huwezi kuyaona moja kwa moja, hapa ndipo unapotakiwa kuwa mwangalifu sana na maamuzi yote yote hasa katika vile unavyovifanya katika maisha yako.

•Utake usitake, maamuzi yoyote yatakupa matunda au matokeo hata kama ni kidogo sana. Hapa sasa ndipo unapotakiwa ujue mafanikio kama mafanikio yanajengwa kwenye mstari mwembamba sana ambao wengi wanashindwa kuutambua.

•Tofauti ya tajiri na maskini ndipo huanza kujitokeza, kwa mfano matajiri hujali sana kupata matokeo yasiyoonekana, tofauti na watu maskini ambao wao hutaka papo kwa papo, hutaka mambo yaonekane tu.

•Kuwa makini sana na mambo unayoyafanya, kila jambo lifanye kwa faida, ili ukianza kuvuna matokeo usiyoyaona miaka kumi ijayo usije ukashikwa na mshangao, kwamba ‘alaa hivi kumbe nilikosea wapi.’

•Ndio maana tunasema hivi hata yale maamuzi unayoyafanya leo, hayana uwezo wa kuathiri maisha yako kesho, kesho kutwa au mwakani, ila matokea ya maamuzi yako unaweza ukaanza kuyaona hata baada ya miaka mitatu, miaka mitano au hata zaidi ya hapo kabisa.

•Kila wakati kuwa makini na maamuzi yako, kuwa na maamuzi ya busara. Kama utakuwa na maamuzi mabovu usishangae ukaja kukuta maisha yako tayari yameshaharibika na itakuwa ngumu sana kwako kuanza upya kurekebisha kwani itachukua muda pia.

•Hakuna wa kukufanya ushindwe au kukuonea kwenye maisha yako. Kila kitu unacho wewe. Tambua kabisa yapo matokeo yasiyoonekana leo kwenye maisha yako, angalia matokeo hayo yasiweze kukupoteza.

•Chunga matumizi yako ya pesa, angalia uhusiano wako na watu wengine, fanya kila unavyoweza kufanya kila kitu kiwe kwa ubora kwako hata kama huna matokeo yasiyoonekana. Matokeo hayo ipo siku yataonekna na yatakuwa nje.

•Sasa usije ukawa miongoni mwa wale watakaolia kwa sababu ya kuvuna matokeo mabovu, ya mambo ambayo hawakutarajia yatakuja kuonekana. Fanya vitu vyenye maana, upate matokeo yanayoonekana mbeleni.