Wednesday, June 23, 2021

Kuna wakati Mungu anakuruhusu kupitia mambo magumu ili baadaye uje kuwa msaada kwa wengine.

Kuna wakati Mungu anakuruhusu kupitia mambo magumu ili baadaye uje kuwa msaada kwa wengine. 


Sio kile unachopitia ni kwa sababu Mungu alikusahau au ulikosea...


...kuna wakati unatumiwa Kama “Specimen” ili wengine wafaidike kupitia uliyopitia.


Kuna makosa umeyafanya ili uje kuwa mwalimu wa wengine wasifanye hayo...


...kuna magumu umepitia na yamekupa maumivu fulani ili uje uwasaidie wengine wasipitie maumivu Kama hayo.


Kuna wakati unaweza ukatamani usiwe “specimen” ya wengine ila ndio hivyo Mungu anakuwa amekuchagua.


Uzuri ni kuwa hawezi akaruhusu upitie mambo kwa ajili ya wengine na wewe akakuacha uwe na mwisho mbaya.


Comment ulichojifunza....


Ilishawahi kukutokea ukawa specimen, share nasi tujifunze...


Share makala hii na Tag na wengine wajifunze...


See You At The Top

 

Friday, May 10, 2019

Kitu kimoja kati ya vitu vya muhimu sana katika ulimwengu huu ni kujifunza kudeal na assignment yako ya wewe kuishi hapa duniani basi! 
Watu sikuhizi wanaacha kufanya ya kwao wanaanza kujadili na kuhukumu maisha ya wengine,utasikia......flani kajiachia sana sikuhizi,flani ni mbea,flani kashinda njaa,flani kabakwa,flani kaachwaa,flani kaibaa,flani sio mwaminifu,flani amekuwa mlevi,flani amebadirika,flani anafanya dhambi kila siku,mambo meeengi ya watu wengine unaacha kutimiza mambo yako, rafiki yangu this world is not our home! 
Huu ulimwengu si nyumbani kwetu kila mtu atakufa na kifurushi chake na atatoa hesabu ya kifurushi chake yeye mwenyewe unapata wapi ujasiri wa kumsema na kumuhukumu mwingine??? Deal na Maisha Yako rafiki!
Una mambo mengi sana ya kufanya ili kutimiza kusudi la wewe kuwepo hapa duniani,wala hujafika hata nusu ya makusudio unapata wapi muda wa kufatilia mambo ya watu???
No matter flani kafanya nn,wewe haikuhusu ilihali haina mashiko kwenye assignment yako basi pambana na kusudi lako, usimseme mtu wala usimfatilie mtu,kumbuka kila mtu anamapungufu yake hivyo hata wewe una yakwako,so pambana nayo.
Mungu ndiye ajuaye maisha ya kila mmoja wetu,acha kukosoa maisha ya wengine pambana kuweka sawa safari ya maisha ya kwako, mengine Mungu atadeal nayo.
Umekaa kila siku mambo yako hayaendi kazi unaongea ya watu tu,tena bora ingekua unaongea kwa wema unaeneza mabaya tu kila siku huchoki???
Tukitafuta la kwako jema hata moja tutalipata???
Huu mwaka hebu badilika basi,achana na maisha ya watu hebu litafute kusudi lako pambana nalo mpaka litimie, watu hawabadilishwi kwa maneno yako bali kwa matendo yako,
Ukifanya vyema kwenye kusudi lako na ukawa mwaminifu huwezi jua unaweza kuwagusa na wengine wakabadilika kuliko kushinda unaongea mambo ya mtu mwingine,kwanza hawezi kukuelewa.......unamwambia mtu afunge kusali wakati wewe hujawahi hata kufunga siku moja, unamwambia mtu aache ulevi huku na wewe unapiga vyombo??
Flani amekengeuka,basi muombee maisha yaendelee,Kijana mwenzako katoka nje ya line muombee maisha yaendelee!
Tujifunze kutafuta kutimiza assignment zetu zilizofanya tukaja kuishi hapa duniani..

Tuesday, April 9, 2019

MWANGA UMEBEBA HATIMA YA MAISHA YAKO!!

MWANGA UMEBEBA HATIMA YA MAISHA YAKO!!


Mwanga hata siku moja huwa hauwezi kushindana na giza.Mwanga una uwezo mkubwa sana kiasi kwamba giza haliwezi kuwa competitor wake. Popote penye giza mwanga ukitokea tu basi giza linakimbia haraka sana na kwenda mbali au kuondoka kabisa. 

Adui wa kwanza kabisa wa Mafanikio ya mwanadamu ni giza lililopo ndani yake. Kukosa maarifa na taarifa sahihi ni kuwa na giza totoro ndani yako.

Mafanikio ya mtu yeyote huanzia kwa kuwa na mwanga kwanza kwenye maisha yake.Huwezi kuona chochote gizani. Huwezi kufanya shughuli yoyote gizani. Huwezi kula, huwezi kusoma,huwezi kuandika, kuwezi kuchukua kitu chochote kirahisi ukiwa gizani. Hata ukiwekewa zawadi kubwa kiasi gani kukiwa na giza huwezi kuona hiyo zawadi.

Mtu anapopata taarifa sahihi na maarifa kuhusu jambo fulani hiyo ndo huwa hatua ya kwanza kabisa ya mafanikio ya huyo mtu kupata alichokuwa anakitaka na mtu akipata maarifa tunasema mwanga umeingia ndani yake na hivyo giza limekimbia. Tunapozungumzia mwanga tunazungumzia kuzitafuta taarifa na maarifa zitakazoondoa giza la ujinga uliopo akilini mwako.

Kukosa maarifa na taarifa chanya kumesababisha masikini wengi duniani kuliko kingine chochote. Vijana wanalalamika hakuna fursa ni kwasababu wana giza ndani yao. Vijana wanalalamika vyuma vimekaza ni kwasababu hawana mwanga ndani yao.

Warren Buffet anasema ukiwa na maarifa na taarifa sahihi ni mwanzo wa wewe kufanikiwa kwani maarifa yanaleta mtaji, maarifa yanaleta mbinu, maarifa yanaleta wateja, maarifa yanavuta fursa, maarifa yanatenegeneza network sahihi. Maarifa yanakuepusha na hasara na kuingizwa mkenge, maarifa yatakuketisha na wakuu, maarifa ndo yatakufanya uvumilie unapopita kipindi cha magumu, maarifa yatakufanya upambane kwa bidii na kujituma.

Kumbuka maandiko matakatifu yanasema "Tunaangamia kwa kukosa maarifa". Kwa maana harisi ni kuwa, watu wanakuwa masikini kwa kukosa maarifa. Watu wanafeli kwenye ndoto zao kwa kukosa maarifa. Watu wanakata tamaa za ndoto zao kwa kukosa maarifa. Kwa kifupi ni kuwa MAARIFA NDO YAMESABABISHA WATU KUFANIKIWA NA WATU KUFELI.

Live Your Dream!!

Mungu Ibariki Tanzania

Monday, February 26, 2018

KUWA NA MOYO WA UTULIVU KATIKA FURAHA

MOYO WA UTULIVU KATIKA FURAHA

Mungu amemuumbia mwanadamu upendo ndani yake ambao muda mwingi anatamani sana kueleza rafiki na ndugu zake kila kitu na jambo zuri linalotokea kwenye maisha yake, atukuzwe Mungu huyo huyo ambaye ameachilia Roho wake ndani yetu katika kutujulisha na kuturuhusu kusema kila jambo kwa watu, yeye awezaye kuruhusu useme kwenye mazingira mazuri anao uwezo wa kukuzuia usiseme njozi zako kwa kusudi maalumu.

Umechumbia/kuchumbiwa sehemu, kaa na Mungu tulia nalo katika furaha ya moyo wako, hadi utakapopata mpenyo wa kulisema hilo jambo, inawezekana kabisa halijafika muda wa kulisema kwa watu, ukisema umeharibu radha kabisa.

Mungu amekusemesha juu ya namna utakuwa siku za usoni kwenye utumishi ulio nao, kazi utakayo kuwa nayo, kanisa litakavyokuwa kubwa kwa utukufu wa Mungu, kaa nalo kwenye maombi, atamia hilo jambo hadi litakapokuwa limekomaa na kuwa tayari, kuku anapokuwa anaatamia mayai yake huwa hana urafiki wa kuku wengine kwa ukaribu wa kuwaamini sana kuku hao.

Yesu alikuwa na wanafunzi kumi na wawili  lakini watatu tu ndiyo walikuwa wanajua siri nyingi za Yesu, wapi anapitia kwenye ugumu, na hata muda mwingine alikuwa akiwaeeleza jambo anawaambia msimwambie mtu yeyote kwa habari ya haya mambo.

Yusufu aliona ufahari sana kuwaeleza ndugu zake juu ya ndoto aliyoiota matokeo yake ndugu zake wakamchukia sana hata Ikafika hatua ya kupanga njama ya kumuua.

NOTE that;

1. Umechukiwa sana kwa sababu ya kufungua ukurasa kwa mtu au watu ambao siyo sahihi kwako na kuwaeleza ndoto zako, unaonekana unajidai wakati ndivyo ULIVYO

2. Si kila mtu anafurahia eneo ambalo Mungu kakuweka

3. Adui pia anatumia watu kukukwamisha

4. Jenga mazingira ya kumsikiliza sana Roho Mtakatifu juu ya nini cha kusema na nini cha kutokusema

5. Ukiona unapata ugumu kusema jambo lolote kwa watu unao waamini, acha hilo jambo haraka sana.

Nimekuombea Mungu akusimamishe katika kusudi lake mahali ulipo katika jina la Yesu

Good day much Love you all....

ZITAMBUWE SIKU HATARI ZA KUPATA MIMBA KWA MWANAMKE

Ili kufahamu vizuri ni siku zipi ni hatari kwa mwanamke kupata mimba,ufahamu thabiti kuhusu mzunguko wa hedhi[menstrual cycle] ni jambo la muhimu sana.

Kwa wastani,mzunguko wa hedhi ni siku 28.
Mzunguko wa hedhi unaanza kuhesabiwa kuanzia siku ya kwanza mwanamke anapoanza ku bleed(label it as day one).

MZUNGUKO WA HEDHI WA KAWAIDA UNA SIFA MADHUBUTI[CHARACTERISTICS OF NORMAL MENSTRUAL PERIOD]

1.IDADI YA SIKU KATIKA MZUNGUKO MMOJA(cycle length)
Kwa kawaida idadi ya siku katika mzunguko ambazo huhesabika kama ni mzunguko wa kawaida ni siku 21 hadi 35 (ambapo hapo ndipo unapata wastani wa siku 28 yaani [(21+35)÷2].
Kwahiyo ndugu msomaji usikariri kuwa mzunguko wa kila mwanamke una siku 28,hiyo ni big no.wengine wana siku 27,wengine 25,wengine 35,wengine 29.

2.SIFA YA PILI NI UWIANO WA IDADI YA SIKU ZA MZUNGUKO KATI YA MZUNGUKO MMOJA NA MWINGINE(REGULAR VS IRREGULAR CYCLES) .
Hii ni miongoni mwa changamoto kubwa sana katika suala zima la ngono kwani inaweza kuwa vigumu kuzitambua siku hatarishi kwa mwanamke kupata mimba.
Ili tuseme mwanamke anamizunguko ya hedhi iliyo sawa[regular cycles],idadi ya siku za mizunguko ya hedhi isitofautiane kwa zaidi ya WIKI MOJA[7 days].
Kwa mfano,kama mwezi wa kwanza aliona siku zake baada ya siku 28,mwezi wapili akaona baada ya siku 30,mwezi wa tatu akaona baada ya siku 35 na wanne akaona baada ya siku 21,bado mzunguko wake uko kwenye uwiano mzuri[regular cycle] kwasababu mzunguko mmoja na mwingine haujatofautiana kwa zaidi ya siku 7.
Usikariri kuwa siku za mzunguko kwa kila mwanamke ni siku 28,hiyo ni big NO.Hiyo 28 ni wastani tu.
Wengine wana bleed kila baada ya siku 21,wengine25 wengine,29,wengine 35 na bado tunasema mizunguko yao bado ni regular[uwiano sahihi].
Pia tambua ya kuwa si lazima idadi ya siku katika mzunguko mmoja ilingane na mzunguko mwingine kwa mwanamke huyohuyo,kwa mfano usitarajie kuwa kama mwezi march ame bleed baada ya siku 28 na mwezi april pia ata bleed baada ya siku 28,sio lazima iwe hivyo lakini pia inaweza tokea.
Kwa mfano mwanamke mzunguko huu anaweza kuona siku zake baada ya siku 28,mzunguko unaofuata baada ya siku 27,mzunguko mwingine baada ya siku 30,mzunguko mwingine baada ya siku 29,mzunguko mwingine baada ya siku 25 na bado yuko kwenye uwiano sawa(tofauti si zaidi ya siku 7).

3.IDADI YA SIKU ZA KUBLEED[MENSTRUAL PERIOD]
Usichanganye kati ya menstrual period na menstrual cycle,hivi ni vitu viwili tofauti kabisa.
Siku ya kwanza ya kubleed ndo siku tunayoanza kuhesabu mzunguko wa hedhi[day one],sio siku ya kumaliza ku bleed. Kwa kawaida idadi ya siku za ku bleed ni kati ya siku 3 hadi 7,kila mwanamke ana idadi yake kati ya hizo.

4. Sifa ya mwisho ya mzunguko wa hedhi ni WINGI WA DAMU inayotoka wakati wa hedhi[amount of menstrual blood],ambapo mwanamke anaweza ku bleed kawaida[normal bleeding] au ku bleed sana[heavy bleeding].

ILI KUZIFAHAMU VIZURI SIKU HATARI KWA MWANAMKE KUPATA MIMBA HEBU TUANGALIE KIDOGO JINSI MAYAI YANAVYOKOMAA NA KISHA KUTOLEWA KWENYE OVARY.
Tufahamu mzunguko wa ovary(ovarian cycle).
Mzunguko wa ovary[ovarian cycle) ndio unaoleta mabadiliko katika mfuko wa uzazi(menstrual cycle).
Mzunguko wa ovary una hatua zifuatazo
Follicular phase,ovulation na luteal phase.

1.FOLLICULAR PHASE: Sehemu hii ya mzunguko huanza siku ya kwanza ya mwanamke ku bleed mpaka yai linapokuwa limekomaa[graafian follicle)
Mayai ya mwanamke huanza kutengenezwa wakati akiwa tumboni mwa mama.
Mpaka kufikia balehe [puberty],mwanamke anakuwa na mayai yapatayo 400,000 ndani ya ovary,mayai haya huwa katika hatua ya uchanga[primary oocyte].

2.OVULATION; katika hatua hii ya mzunguko wa ovary,yai lililokomaa[graafian follicle] hutoka kwenye ovary na kuingia kwenye mirija ya fallopian.
Sasa tutaitambuaje siku ya yai kutoka[ovulation]?.
Kiuhalisia ni ngumu kujua siku halisi yai lilipotolewa lakini tunaweza kuzitambua siku nyeti ambazo zitatupa nafasi kubwa ya kutokulikosa yai ndani ya siku hizo.Fuatilia hapo chini.

3.LUTEAL PHASE : hii ni sehemu ya mzunguko wa ovary ambayo huanza baada ya yai kutoka[ovulation] na kuishia kabla ya kuanza ku bleed[mwanzo wa mzunguko mwingine).
ZINGATIA HAPA, idadi ya siku kati ya ovarian cycle na menstrual cycle ni sawa[mfano,28,30,35,25).
Idadi ya siku katika luteal phase ni sawa kwa mizunguko yote na ni siku 14.

ANGALIA HESABU HII RAHISI
Folicular phase +luteal phase =Idadi ya siku katika mzunguko[the cycle length).
Lakini tayari tumeshajua luteal phase ni constant,haibadiliki,[ni siku 14 katika kila mzunguko].ovulation phase hapo iondoe maana ovulation hutokea masaa machache tu.
Sasa ili kuipata siku ya ovulation,tunachukua idadi ya siku katika mzunguko mmoja - idadi ya siku katika luteal phase,ambayo haibadiliki[14 days].
Kwa mfano kwa mwanamke mwenye mzunguko wa siku 28,kuipata siku ya ovulation tunachukua 28-14 tunapata 14,kwahiyo kutoka siku ya kwanza mwanamke alipoanza kubleed ni siku ya 14 ndipo yai linakuwa tayari kurutubishwa.
Kwa mwenye mzunguko wa siku 30, tunachukua 30-14(luteal phase)=16,kwa hiyo mwanamke mwenye mzunguko wa siku 30,ovulation inauwezekano mkubwa wakutokea siku ya 16 na si ya 14(kuwa makini hapo).
Yule mwenye mzunguko wa siku 35 ,ovulation day ni 35-14 = 21,kwa hiyo kwa mwanamke mwenye mzunguko wa siku 35,ovulation ina nafasi kubwa ya kutokea siku ya 21 na si ya 14.
Sasa baada ya kuijua siku ya ovulation lazima uwe makini na siku zinazokaribiana na siku ya ovulation kwani nazo ni siku hatari pia.
KWANINI?

Mbegu ya kiume inauwezo wa kuwa hai hadi masaa 48 (2 days) tangu shahawa zimwagwe[ejaculation] na yai lina uwezo wa kuwa hai hadi masaa 24[one day] tangu lilipotoka kwenye ovary.
Kwaiyo kama mwanaume akijamiiana na mwanamke siku mbili kabla ya yai kutolewa kwenye ovary, mbegu inaweza kuwa hai bado na kutungisha mimba endapo yai litatolewa ndani ya siku mbili zijazo kwa mfano kama siku ya ovulation ya mwanamke ni siku ya 14, mwanamke akijamiiana na mwanaume siku ya 12, uwezekano wa kupata mimba ni mkubwa.
Kadhalika kama mwanamke ametoa yai siku ya 14 kisha akajamiiana ndani ya masaa 24 mbele, pia anaweza kupata mimba kwasababu kipindi mbegu zinamwagwa zinaweza kulikuta yai bado lipo hai na kutungisha mimba.
Kwa ufupi,ni siku tatu tu ndizo hatarishi sana kwa mwanamke kupata mimba,yaani,siku mbili kabla ya ovulation na ndani ya masaa 24 baada ya ovulation[narrow but dangerous window].
Kwa kuongezea,kipindi cha ovulation mwanamke anapata nyege kali sana kwasababu ni kipindi ambacho kuna homoni fulani[androgens] ambazo huchochea nyege huzalishwa kwa wingi. Pia kipindi hicho cha ovulation au karibia ovulation joto la mwili la mwanamke hupanda,anajihisi mwili kuchemka tofauti kidogo na ilivyo kawaida yake.

SASA BASI KWA KUWA NIMESEMA HATUWEZI KUWA NA UHAKIKA WA 100% WA SIKU YA OVULATION NDO MAANA HUWA TUNATUMIA KANUNI YA KUEPUKA NGONO KWA KIPINDI CHA WIKI NZIMA[7 DAYS] AMBAZO NI SIKU ZILIZO KARIBU SANA NA SIKU YA OVULATION KWA WALE WANAOTUMIA CALENDER METHOD.

Mfano,kama una mzunguko wa siku 30, kuipata siku ya ovulation chukua 30- 14=16,kwa hiyo siku ya ovulation ni ya 16 tangia ulipoanza kuona damu siku ya kwanza.sasa kama ni siku ya 16,ondoa siku nne kabla ya hiyo siku ya ovulation.kwahiyo kuanzia siku ya 12 hapo,acha ngono.
Pia jumlisha siku 3 mbele,ambapo mwanamke atatakiwa kuanza ngono kuanzia siku ya 19 huko ili kuepuka mimba.

Friday, January 26, 2018

JE, NIINGIE KWENYE MAISHA YA NDOA NA NANI?

JE, NIINGIE KWENYE MAISHA YA NDOA NA NANI?

Wengi limekuwa jambo gumu sana kutaka kujua aingie kwenye maisha ya mahusiano na ndoa bdae na mtu gani, unisikilize itakusaidia.

1. Hakikisha mtu huyo anamcha BWANA.

Wewe siyo Yesu hadi uokoe, si swala la kuingia na mtu asiyemcha BWANA ukidhani uko salama, maandiko yanasema tusifungiwe nira na mtu asiye amini.

Kuamini nini, kuamini imani ya Kristo Yesu

Neema ya wokovu bado ipo, utashangaa utakapoamua kukubali kuiingia kwenye maisha na mtu asiyeamini imani yako ghafla ameshakuweka ndani anakugeukia, anakwambia kuanzia leo hakuna kwenda kanisani, anakuchekea leo, kesho atakugeuka, moyo wa mwanadamu kama haumjui Mungu ni hatari sana...

Tukumbushane kidogo hapa wapendwa "Kilichomfanya Yusufu amkimbie yule mama mke wa potifa bila kufanya nae dhambi, ilikuwa ni neema ya kumjua Mungu iliyokuwepo juu ya Yusufu", Sasa fikiria ndiyo imemtokea boyfriend wako ambaye hamjui Mungu, kitu gani kitatokea..? (Jitafakari moyoni mweyewee hata usichekee)

Weit my friend God's Fearful relationship itakusaidia kukutunza hata kama mwili utainuka, utastahimili usimtende Mungu dhambi kwa sababu tu ya neema ya kuwa na hofu ya Mungu baina yako na mtu uliyepo kwenye mahusiano, ila kama mmoja hofu ya Mungu haipo, uwe na uhakika hamtaweza kustahimili, trust me.

Mabinti wengi wanaomjua Mungu waliopo makanisani, asilimia kubwa hawako tayari kuolewa na vijana wa kanisa, why,.

Vijana wa kanisani wanaonekana washamba sana, watu wa mabwanga, asante Yesu nilizungumza sababu zinazopelekea wakaka kuachika sana, likiwemo hilo.

Suluhisho.

Mueleze kwa hekima, vaa shati linalokutosha vizuri, vaa suluari zinazokuenea vzr

Akikataa, tulia kwanza, rudi tena, maana ni wabishi kubadili kwa haraka haraka, muombe Mungu akusaidie hadi aelewe.

Nia yangu ni hii, usimuache mkaka kisa anavaa mabwanga, ndiyo maana upo umsaidie awe smart, ili uanze kumtambulisha bila aibu kwa marafiki zako.

2. Mwenye kujua nini anapaswa kufanya kwa mwenzake kutimiza kusudi la yeye kuwa na mwenzake.

3. Aliye tayari kujifunza, kuongozwa na mwanaume huyo, kama haupo tayari kujifunza kwake na kuongozwa naye kama kiongozi wa familia, usikubali akuoe, muache atafute mwingine.
Usikubali kama haupo tayari kuwajibika kwake​,
Usikubali kama unaona anapwaya kwenye vigezo vyako, yaani siyo shauku ya moyo wako, usikubali kuwa naye, muache atafute mwingine​.

4. Hakikisha amani ya moyo wako kutoka ndani kabisa imekubali kwenda na mtu huyo, yaani mkaka huyo, usiingie nae kisa ana kibanda cha chipsi mayai, usikubali kisa ana kioski, usikubali kisa ana salon ya wadada, usikubali kisa ana gari, usikubali kisa ana nyumba, upendo haujengwi kwa vitu, uwe na uhakika ndani yako uhalisia unakataa, upendo unakuja automatic, love without any reason will sustain your relationship.

Friday, January 19, 2018

YAJUE MAMBO AMBAYO MWANAUME YEYOTE ANAYOYAHITAJI.

YAJUE MAMBO AMBAYO MKAKA YEYOTE ANAYOYAHITAJI.
Madada (Wanawake) wengi wanahisi wanawafahamu sana wakaka, sikatai ila wengi wao wanawafaham kwa sehemu tu, ukitaka kuishi na mtu vizuri jenga nidhamu ya kumfahamu, na huwez kumfaham bila kwenda kwa aliyemuumba kwanza katika kitabu cha mwanzo, tambua ni vitu gani Mungu aliviweka ndani yake. 

Mkaka yeyote yule, ni mshamba au mjanja, ni msomi au mpoli poli, ameokoka hajaokoka, ni mfupi au mrefu, ni mweupe au mweusi, ana kitambi au hana, wote hawa kwa makundi yao wanahitaji sana sana kitu kinaitwa ​KUHESHIMIWA​ hilo jambo likikosekana, utaona mkaka anaanza kuwa na hasira kama mbogo, why anatetea nafasi yake kuporwa, nafasi ipi nafasi ya kunyimwa heshima yake.
Ukiona unakaa na mkaka mwezi mmoja ghafla anapotea kimya kimya, chunguza maneno yako kwake, huyo siyo mdada mwenzako ujue, unamzodoa amekuwa mdogo wako? amekuwa mdada mwenzako? silaha ya mwanamke mwenye akili ya kulinda nyumba yake yuko makini sana katika kufungua kinywa chake.

Hata kama Yesu kaongea na wewe mengi juu yako katika mahusiano yako, unahitaji nidhamu sana katika kuongea nae, wengi wameachwa kwa ajili ya dharau na kiburi, mdada yeyote mwenye kiburi chunguza mwisho wake, ni kuachika kila kukicha
Ndiyo maana unaweza kuona wakaka wengi waliookoka utakuta wanammendea mdada mmoja kwenye fellowship, why, kitu gani wameona, ​HESHIMA​ ukiona wakaka hawakatizi kwako cha kwanza omba Mungu aondoe mtazamo wanaouona juu yako ya kiburi ili akupe hekima inayoleta nidhamu ya heshima kwa mkaka, huamini endelea na kiburi chako uone kama kuna mkaka atapata shauku ya kuwa na wewe.

Mungu awabariki sana wadada wote wenye heshima, mjue uzuri ni ubatili bali mwanamke amchaye Bwana huyo ndiye atakayesifiwa .
Somo ni refu, sijaanza kufundisha hapo, huo ni utangulizi tu.
Chuoni huwa tunauliza watu waliotutangulia juu ya taarifa muhimu za mwl, nini huyo mwl anataka, je huwa anatabia za kubana course work? je anapenda uandike sana maelezo? au hataki maelezo sana? je anatoaga mekapu? yote hiyo ni ili kuenda naye vizuri baada ya kumfahamu, ninachohofia wengi hukumbuka shuka wakati wa asubuhi, means TOO LATE, fahamu sana mambo ambayo mkaka anayahitaji, mkaka mbona utafurahia tuuu? yajue tu, leo nimeongelea point moja tu. Nitawaletea point wakati mwingine poin nyingine .