Sunday, June 11, 2017

MAFANIKIO HAYAHITAJI KUOMBA RADHI, KUSHINDWA HAKUNA VISINGIZIO.

📖MAFANIKIO HAYAHITAJI KUOMBA RADHI, KUSHINDWA HAKUNA VISINGIZIO.

Ustahimilifu na akili iliyofunguka ni mahitaji ya kivitendo kwa muotajindoto wa leo. Wale ambao ni waoga wa mawazo mapya hushindwa kabla hawajaanza. Haijawahi kutokea wakati muafaka zaidi kwa waasisi  kushinda sasa. Kuna biashara nyingi zisizomithilika, dunia ya kifedha na kiviwanda kuumbwa tena upya na kuelekezwa sambamba na njia mpya zilizokuwa bora zaidi.

Katika kupanga kupata mgawo wako wa utajiri, usiruhusu mtu akushawishi kumdharau muotajindoto. Kuvishinda vigingi vikubwa katika hii dunia inayobadilika kila wakati, ni lazima uwe na roho ya waasisi wakubwa wa zamani ambao ndoto zao zimeupa ustaarabu kila kitu cha thamani uliyokuwa nacho, roho ambayo hutumikia mithili ya damu ya uhai wa jamii yetu-nafasi yako na yakwangu, kuendeleza na kutafuta soko la vipaji vyetu....... #Napolian Hill

Tusisahau, Columbus aliota juu ya Dunia isiyojulikana, akihatarisha maisha yake kwa uwepo wa dunia hiyo, na aliivumbua! Copernicus, mwana-elimu ya anga, aliota juu ya uwepo wa sayari nyingi, na hilo alilithibitisha! Baada ya kusherekea ushindi hakuna mtu aliyemshutumu hadharani kuwa aliyoyasema yalikuwa hayatekelezeki. Badala yake Dunia ilitoa heshima kubwa kwenye kaburi lake, hivyo kuthibitisha kwa mara nyingine tena kwamba, mafanikio hayahitaji kuomba radhi, kushindwa hakuna kisingizio.....

#Nice week end...
#Nice Sunday....
#Nice day...